Plus 255 Studios

Plus 255 Studios
Home » » KATIBA: FIKRA KOMAVU ZA HUMPHREY POLEPOLE

KATIBA: FIKRA KOMAVU ZA HUMPHREY POLEPOLE



TUKATAE HADAA, SERIKALI YA TANGANYIKA HAIPASWI KUFICHWA KATIKA SERIKALI YA MUUNGANO NA ZANZIBAR INAPIGWA TEKE PEMBENI, WAISHIO ZANZIBAR NI WATANZANIA WENZETU. MIMI NINAKATAA HADAA HATA KAMA NIKO PEKE YANGU.
Katiba Inayopendekezwa ya Mhe. Chenge, inatugawa watanzania. Ukiacha Mbinguni hapa duniani nina Tanzania tu, sitakubali ubaguzi. Katiba ya Muungano inapaswa kuwa ya Muungano na si ya Tanganyika pekee.
IKUMBUKWE kuwa Vifungu vya Katiba husomwa kwa pamoja, ukiona ulipendalo limekaa sawa lakini hujali maeneo mengine, wewe huna tofauti na wabinafsi wale wale. Rasimu ya Katiba Inayopendekezwa UBORA wake ni UJUMLA wake.
1. Vijana mkifurahia Baraza la Vijana ndani ya Katiba ilhali Muundo ni mbaya na mnajua Baraza hilo ni kwa Tanganyika pekee, huo ni ubinafsi, mmewatenga vijana wenzenu wa Zanzibar. Na mkumbuke changamoto za vijana hazitaondolewa na Baraza la vijana. Jiulizeni kama Katiba hii ni ya wananchi, mbona Baraza la Wanawake hakuna maana wenye shida zaidi ni wanawake na ndio wengi kwa idadi, mbona Baraza la NGOs halijawekwa. Mimi ni kijana na sikubali kuhadaiwa, Mambo hayo sio ya Muungano na hayapaswi kuwa katika Katiba ya Muungano.
2. Wakina mama zangu msifurahie 50/50 mkaridhika ilhali mkijua muundo wa Bunge la Muungano una matatizo, wakati mkijua fika hayo mambo ya wanawake hayatekelezwi kimuungano, je mmekuwa wabinafsi kiasi hiki kwamba wanawake wenzenu wa Zanzibar hamuwajali. Ama ndio shida yenu ikionekana kuanza kuondoka shida ya wenzako si yako? Tafakarini wamama na dada zangu, katika hili tuko pamoja. Tusiwapongeze ilhali tunajua dhamira yao si safi.
3. Wasanii wa tasnia mbali mbali ni kweli kazi yenu imeisha? La hasha. Katiba ni kama mwili wa Binadamu, Mwili umekuwa unaumwa kwa muda mrefu, sasa tunaupatia tiba kwa ujumla wake, hivi mdogo na masikio ukionekana kuelekea kupona utapuuza maumivu ya kichwa, miguu, mikono, macho, mgongo, tumbo na sehemu nyingine za mwili? tena la hasha, mambo ya wasanii hata leo hayatendewi kimuungano, mbona hatuwahoji akina Mhe. Sitta na Chenge, kwanini tunaweka mambo ya Tanzania Bara katika Katiba ya Muungano na tunayaita ya wananchi wa Tanzania. Hatutakuwa tumepona kama tutaridhika kwetu kuna amani na kwa jirani kunawaka moto. Mimi ni msanii, ni mchoraji na nimesoma uchoraji kwa miaka 10, mimi ninapiga gitaa na ninapenda kuimba, ila nakataa hadaa.
4. Wakulima ninyi ndio mnasukuma kwa kiasi kikubwa gurudumu la uchumi wa Nchi yetu. Wanasema wameweka mambo ya wakulima sawa. Niwaambize mama, baba, dada, kaka, rafiki na ndugu zangu, Kilimo sio jambo la Muungano tangu tuungane mwaka 1964. Iweje leo wawaambie mambo yenu yapo katika Katiba ya Muungano wakati kiutendaji ni kwa watanganyika pekee. Sidhani kama wakulima ni wabinafsi kwamba maadamu mambo ya wakulima wa tanzania bara wamekaa sawa, mtapuuza wakulima wa mwani, karafuu na mpunga kule Zanzibar.
NINAENDELEA
..............haija haririwa............

0 comments:

Post a Comment