Plus 255 Studios

Plus 255 Studios
Home » » Wananchi wazuia msafara wa JK

Wananchi wazuia msafara wa JK



Njombe. Wananchi wa Kijiji cha Makoga Wilaya ya Wanging’ombe mkoani Njombe jana walisimamisha msafara wa Rais Jakaya Kikwete na kumweleza kero zao mbalimbali ikiwamo ya kutaka gari la kubebea wagonjwa (ambulance) kwa ajili ya zahanati ya kijiji hicho.
Wananchi hao walifurika saa nne asubuhi kandokando ya barabara na kuomba msafara wa Rais Kikwete usimame.
Msafara wa Rais Kikwete ulikuwa unatokea Makete kuelekea Njombe na ndiyo ukakutana na wananchi hao waliokuwa na shauku ya kueleza matatizo hayo kwa Rais.
Rais Kikwete alikubali kushuka na ndipo baadhi ya wananchi mmoja mmoja wakaanza kutaja kero zinazowakabili katika Kijiji cha Makoga.
Wananchi waliomba kuboreshwa kwa huduma ya maji pamoja na kuwahishiwa pembejeo za kilimo.
“Mheshimiwa Rais pia tunaomba gari la wagonjwa kwani tunapata shida sana kuwapeleka wagonjwa wetu hospitali,” alisikika mmoja wa wananchi hao akisema.
Majibu ya Rais Kikwete
Akijibu kero hizo za wananchi, Rais Kikwete aliwaahidi kuwa Serikali yake itatafuta fedha kwa ajili ya kuwaletea gari la wagonjwa.
Kuhusu pembejeo za kilimo, alisema Serikali itaangalia uwezekano wa kuongeza pembejeo za kilimo mwakani. Kuhusu maji alisema kijiji hicho kipo kwenye mpango wa vijiji 10 vitakavyopatiwa huduma ya maji katika Halmashauri ya Wilaya ya Wanging’ombe katika bajeti ya mwaka 2013/14.
Pia Naibu Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene alisema kijiji kipo kwenye mpango wa kuletewa umeme hivi karibuni.
Ahimiza tohara
Pia Rais Kikwete aliwataka wanaume nchini kuendelea kujitokeza kwa wingi kupata tohara kama moja ya njia za kukabiliana na ugonjwa wa Ukimwi.

 THE ENQUISITOR

0 comments:

Post a Comment